Marehemu Prudhomme aliyekuwa ameandamana na binti yake kujiburudisha, alipelekwa nyumbani akiwa mlevi chakari.
Inaarifiwa kuwa alikimbizwa hospitalini ambapo alipatikana ameaga dunia siku iliyofuatia.
Hata hivyo mahakama ilimpata na hatia mhudumu huyo Gilles Crepin, mwenye umri wa miaka 47, kwa kumchochea marehemu Prudhomme aendelee kubugia mvinyo ilihali alikuwa mlevi kupindukia.
Mahakama ilisema kuwa Crepin aliendelea kuandika nani anayeshikilia rekodi hiyo kwenye ubao uliotundikwa hadharani kwa wateja wake.
Sasa Crepin amehukumiwa kifungo cha nyumbani cha miezi minne,na kupigwa marufuku ya kufanya kazi katika baa yeyote kwa kipindi cha mwaka mmoja.
0 comments:
Post a Comment