Ukitaja mbu, wazo litakalomjia mtu kwa haraka ni ugonjwa wa
malaria.
Hiyo inatokana na mazoea yenye ukweli kwamba, mdudu huyo hueneza ugonjwa huo kama ilivyo kwa malale na matende.
Hiyo inatokana na mazoea yenye ukweli kwamba, mdudu huyo hueneza ugonjwa huo kama ilivyo kwa malale na matende.
Lakini kuna baadhi ya mambo kuhusu tabia ya mbu
ambayo watu wengi hawayafahamu, mbali na sifa yake ya kueneza
magongwa, hasa malaria.
Hebu jiulize; hivi umewahi kukaa na wenzako watano
lakini ukajikuta ni wewe peke yako ndiye unayelalamika kwamba
unang’atwa na mbu?
Kama umekutwa na hali hiyo, basi unaweza kuwa mmoja wa watu walio kivutio kwa mbu.
Wanasayansi wanasema kwamba mtu mmoja kati ya
watano huwa kivutio cha mbu na kwamba mdudu huyo akinusa harufu ya mtu
huyo, hata akiwa na wenzake zaidi wanne, basi atakwenda kwake na kwamba
hata akifukuzwa, mbu huyo atarudi na kumuuma tena mtu huyo.
Daktari bingwa wa upasuaji wa Marekani, Joseph
Mercola anasema kuwa kuna aina nyingi za mbu, lakini asilimia kubwa ya
mbu wenye tabia hiyo ni mbu jike aina ya Anofelesi, ambao pia huambukiza
malaria.
Anasema kuwa mbali na tabia hiyo mbu hao huvutiwa
na maeneo yenye kemikali kwa kunusa harufu hiyo umbali wa mita 50
kutoka walipo kabla ya kwenda kwenye eneo hilo. Mbu jike ndiyo huvutiwa
zaidi na kupenda kunyonya damu ya binadamu kuliko mbu dume.
Dk Mercola ambaye ameandika majarida mbalimbali ya
afya, anasema kuwa mbu jike hupendelea kufanya hivyo kwa sababu madini
ya chuma na protini wanayonyonya kwenye damu ya binadamu huwasaidia
kutengeneza mayai na baadaye kuzaliana.
Kutokana na hilo, wanasayansi wamebaini kuwa mbu huvutiwa na bakteria.
Wanasema binadamu ana bakteria trilioni moja
kwenye ngozi, lakini kati ya hao, asilimia 10 tu ndiyo hufanana kwa
binadamu wote na asilimia nyingine hutofautiana, hali ambayo huchangia
baadhi ya watu kuumwa zaidi na mbu kuliko wengine.
0 comments:
Post a Comment