Friday 1 May 2015

Wanafunzi wapewa mafunzo ya kijeshi nchini Uganda….



Wanafunzi wa shule za msingi nchini Uganda,wamepewa mafunzo ya kijeshi kama njia ya kupambana na kundi la ash Shabab la Somalia.

Mtandao wa habari wa "Africa Times" umeripoti kuwa, wanafunzi wa shule za msingi nchini Uganda wanaandaliwa kijeshi kwa ajili ya kupambana na kundi la ash Shabab.
Kundi la ash Shabab ambalo linaaminika kuwa na wapiganaji elfu sita huko Somalia, ni tishio kwa Uganda.
Msemaji wa serikali ya Uganda Ofwono Opondo,amesema wanamgambo wa ash Shabab hawawalengi wanajeshi pekee,hivyo kuna haja kwa wananchi kupewa mafunzo ya kuweza kupambana na wanamgambo hao.

0 comments:

Post a Comment