Monday 11 May 2015

Ajabu lakini kwelii: Riport ya Gari Zilizotembea miezi 8 bila dereva..!!!!!


Teknolojia imeendelea kusababisha kuonekana kwa maajabu mbali mbali Dunia,yakiwemo ya mambo ambayo kwa kufikiria kwa wepesi kabisa utaona hayawezekani lakini Teknilojia imeyafanya yawezekane.



Moja ya mambo hayo ni pamoja na ile ya mwaka 2014 ambayo ilikuwa gumzo baada ya kutengenezwa magari ambayo yanajiendesha yenyewe bila dereva.

Google pamoja na makampuni mengine yaliamua kuweka nguvu kwenye ubunifu huu, naambiwa mwezi September 2014 California Marekani iliruhusu magari hayo yaendelee kutembezwa katika barabara za kawaida ambazo zinatumiwa na magari mengine pamoja na watu.

Ripoti iliyotoka leo May 11 2015 inaonesha kuwa katika magari 50 ambayo yanatembea bila dereva California, zimewahi kutokea ajali nne tu ambazo zinahusisha gari hizo,japo Google wanasema ajali ambazo zilitokea ni ajali ndogo tu za kawaida.
Ripoti hii ni kama inatia ushawishi wa nchi nyingine kuvutiwa na huu ubunifu na kuanza kutumia aina hii ya magari.

Kingine kilichopo njiani ni hili lori ambalo nalo liko njiani kuja, nalo linatembea bila dereva.


0 comments:

Post a Comment