Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro,amesema
wanaotekeleza mauaji dhidi ya raia katika eneo la Kibiti mkoani Pwani wametumwa
vibaya, na wao watapelekwa vibaya vibaya.
Sirro alisema hayo jana Dar es Salaam kabla ya kukabidhiwa
magari manne na Kampuni ya Great Wall Motor and Haval Company kutoka nchini
China yatakayotumiwa na jeshi hilo.
“Tatizo la mauaji ya raia huko Kibiti na maeneo mengine
nchini, nataka kusema si kawaida yangu kuongea sana, ila sio muda mrefu
yatakwisha, hadi sasa tunakwenda vizuri na wale ambao wametumwa kutekeleza mauaji
hayo wataona majibu yake,” alisema Sirro.
Pia aliwataka viongozi wa vijiji na Serikali za mitaa nchini
kote kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo na kuunda vikundi vya ulinzi shirikishi
ili kukabiliana na wimbi la uhalifu.
Tangu wahalifu kuanza
kutekeleza mauaji kwenye maeneo ya Kibiti na Mkuranga mkoani Pwani, zaidi ya
watu 30 wamefariki dunia wakiwamo askari polisi zaidi ya 10, viongozi wa
Serikali za vijiji na kata.
Jeshi la Polisi
limekuwa likiendesha operesheni maalumu kwenye eneo hilo na mara kadhaa
limetangaza kupambana na wahalifu hao na kufanikiwa kuua baadhi yao
0 comments:
Post a Comment