Wakati Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu, akiwa
bado anakabiliwa na kesi kadhaa za
uchochezi, amefytuka tena na kutoa maneno mazito juu ya viongozi wa Serikali,
huku akisema kwa mujibu wa sheria za nchi, anaweza kukamatwa, lakini si
kufungwa.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari
uliofanyika Dar es Salaam jana, Lissu pia alisema amepata taarifa kutoka kwa
mmoja wa askari polisi kuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, atafikishwa
mahakamani wakati wowote kutokana na kauli alizozitoa juu ya masheikh wa
Uamsho.
Akizungumzia taarifa za Lowassa kufikishwa
mahakamani, alisema amezipata kutoka kwa mmoja wa maofisa wa ngazi za juu ndani
ya Jeshi la Polisi.
Lissu alisema kuwa aliwasiliana na ofisa huyo jana
asubuhi na kumtaka ajiandae kwa kesi hiyo ambayo ipo mbioni kupelekwa
mahakamani.
“Nina taarifa
nimeambiwa leo na lipolisi likubwa kabisa, maana hata wao hawafurahi sana, nimeambiwa
jiandaeni mheshimiwa Lowassa atafikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa uchochezi
kwa sababu ya kuzungumzia uonevu wanaofanyiwa masheikh wa Uamsho,” alisema
Lissu.
Alipoulizwa endapo kinga za kushtakiwa kwa viongozi,
inawahusu pia mawaziri wakuu wastaafu, alisema kinga inamuhusu rais aliyepo
madarakani pekee na mambo aliyofanya wakati akiwa Ikulu.
0 comments:
Post a Comment