Mwanamke
aliyesambaza kanda yake ya video akiikojolea bendera ya Marekani ametoa wito
kwa watu kutoilenga familia yake akisema hawaungi mkono tendo lake.
Emily Lance alipokea vitisho vya
mauaji katika mtandao wa kijamii na ubakaji baada ya kuchapisha kanda hiyo ya
video siku ya uhuru wa taifa hilo.
Akaunti yake haiko tena katika
mtandao wake wa facebook lakini awali alikuwa amechapisha kwamba babake na eneo
analofanya kazi pia limelengwa, kulingana na ripoti.
Kutoheshimu bendera ya Marekani
sio kinyume cha sheria kutokana na sheria nyingi na uhuru wa kujieleza.
Katika kanda hiyo ya video, Bi
Lance anaonekana akisimama juu ya choo ambapo bendera ya Marekani imewekwa na
kuikojolea kupitia usaidizi wa chombo ambacho kinawasaidai wanawake kufanya
hivyo wakiwa wamesimama.
Chini yake aliandika maneneo ya
kuitusi bendera hiyo.
Baadaye aliwataka wanaopinga wazo
lake kutowalenga watu wasio na hatia akisema hakuna hata mtu mmoja katika
familia yake anayeunga mkono wazo lake.
0 comments:
Post a Comment