Jitihada za serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John
Magufuli za kupambana na rushwa, zimewafanya wananchi kuamini kuwa hivi sasa
vitendo hivyo vinapungua kulinganisha na miaka
iliyopita.
Hayo yamebainika kutokana na utafiti uliofanywa na Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam UDSM, kupitia Idara ya Sosholojia kwa kushirikiana na
taasisi inayojishughulisha na masuala ya utawala ya Basel Switzerland.
Akizungumza jijini Dar es Salaam baada ya kuzindua utafiti
huo uliofanywa mwaka jana katika mikoa ya Dar es Salaam na Kagera, Mtafiti
Msaidizi wa UDSM Egidius Kamanyi amesema kuwa, katika kipindi cha nyuma tatizo
la rushwa lilikuwa linachukuliwa kawaida katika jamii tofauti na ilivyo sasa.
Amesema katika utafiti huo wamebaini kwamba kwa sasa jamii
inaogopa kwa kiasi kikubwa kujihusisha na rushwa kuanzia katika huduma ndogo
ndogo hadi kubwa.
Amesema katika utafiti huo wamebaini kwa sasa kila mmoja
anaogopa kujihusisha nayo na kwamba huduma nyingi zinapatikana kwa urahisi
pasipo usumbufu tofauti na ilivyokuwa nyuma hususani katika sekta ya afya.
0 comments:
Post a Comment