Monday 10 July 2017

MSD YABADILI VIFUNGASHIO VYA DAWA…

Bohari ya Dawa (MSD) imetangaza kubadilisha vifungashio vya dawa kutoka kwenye vifungashio vya
makopo kwenda kwenye vifungashio vilivyo kwenye mfumo wa blister Pack ili kuzifanya dawa ziwe salama zaidi kulingana na maelekezo ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).
Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu alisema mwishoni mwa wiki kuwa, kwa muda mrefu MSD ilikuwa ikiuza dawa ambazo ziko kwenye vifungashio vya makopo ambapo watoa huduma huwapimia wagonjwa kiasi cha dawa wanachokihitaji na kisha kuwawekea kwenye vifungashio vya dawa.
“Kuanzia mwaka huu wa fedha MSD imeanza kuagiza dawa kutoka kwa wazalishaji zikiwa zimefungwa kwenye mfumo wa blister pack, dawa hizo sasa zitamwezesha mtumiaji kuzitunza kwa hali ya usafi na usalama zaidi kwa mujibu wa miongozo ya utunzaji dawa,” alisema Bwanakunu.
Vifungashio vya makopo vilikuwa na changamoto kadhaa na huko nyuma, TFDA iliwahi kubaini dawa za kupunguza makali ya ukimwi zikiwa zimewekwa kwenye vifungashio vya makopo vya dawa huku makopo hayo yakiwa tofauti na vifungashio vya dawa vilivyosajiliwa na TFDA.

0 comments:

Post a Comment