Serikali
nchini Uganda imewapiga marufuku wanawake wanaofanya kazi katika ofisi za Umma
kuvaa nguo fupi na zile zinaoonesha miili yao.
Wafanyikazi hao wameambiwa kuwa ni marufuku uvaa mawazi
yanaonesha mapaja, sehemu ya matiti yao.
Agizo hili si tu kwa wanawake,wanaume pia wametakiwa
kuvaa nguo za mikono mirefu, tai na kutovaa suruali za kushuka.
Pamoja na hilo, wanaume wametakiwa kukata kucha na nywele
zao kuwa fupi lakini pia kuepuka kuvaa nguo zinazo ng'aa.
Wizara ya Utumishi wa Umma imesema wafanyikazi
watakaokwenda kinyume na masharti haya watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Aidha Wizara hiyo imesema wanawake wanaweza kuvaa suruali
lakini isiwe ya kubana lakini pia sketi isiwe fupi.
Ripoti zinasema kuwa kanuni hizi zimekuwepo tangu mwaka
2010 lakini zimekuwa hazitekelezwi.
0 comments:
Post a Comment