Mashirika mawili
ya ndege ya Kuwait Airways na Royal Jordanian, yameruhusiwa kuruhusu abiria wake
kubebea laptop ndani ya ndege zinazoelekea Marekani.
Mashirika hayo mawili yamesema yameshirikiana na
maafisa wa Marekani kuimarisha usalama kwa ndege zinazotoka nchini Kuwait na
Jordan.
Marekani ilitangaza marufuku hiyo mwezi Machi kwa
safari za moja kwa moja kutoka nchi nane za kiislamu, kutokana na hofu kuwa
mabomu yangebebwa ndani ya vifaa hivyo.
Mashirika ya ndege ya Etihad, Turkish Airlines,
Emirates na Qatar yaliondolewa marufuku hiyo wiki iliyopita.
Shirika la
Royal Jordanian ambalo hufanya safari katika miji mitatu ya Marekani kutoka
Amman mji mkuu wa Jordan, liliondoa marufuku hiyo baada ya hatua mpya za
kiusalama zilizochukuliwa kwenye ndege zinazoelekea nchini Marekani.
Shirika linalomikiw na serikali la Kuwait Airlines
ambalo hufanya safari zake kutoka Kuwait kuenda mjini New York likipitia
Ireland, limesema marufuku hiyo ilitolewa baada ya maafisa wa Mareknian,
kukagua usalama kwenye safari zake.
0 comments:
Post a Comment