Wakati
ulimwengu ulipoadhimisha siku ya idadia ya watu duniani mwanamume mmoja alikuwa
na sababu 100 za kusherehekea.
Kofi Asilenu mwenye umri wa miaka
80 ni baba wa watoto 100 na wake 12.
Anaishi na familia yake katika
kijiji cha Amankrom kilicho umbali wa kilomita 45 kutoka mji mkuu Acca.
Familia yake ni thuluthi moja ya
watu 600 katika kijiji hicho.
Anasema kuwa anataka familia
kubwa kwa sababu hakuwa na ndugu.
Amesema hana kaka wala shangazi,ndio sababu aliamua kuwa
na watoto wengi ndio wapate kumpa maziko yaliyo mazuri siku akifariki.
Ameongeza kuwa familia hiyo
imemgharimu pakubwa,kwani alikuwa mtu mwenye mali nyingi, lakini male hiyo
ilipungua kutokana na gharama ya kuitunza familia yake kubwa
Kofi Asilenu anaonekama kuwa
mwenye afya nzuri na hata anasema kuwa anataka kuwa na watoto zaidi.
0 comments:
Post a Comment