Mwalimu wa somo la Baiolojia katika
shule ya sekondari ya wasichana ya St Therese mjini Lusaka ambaye alidakwa
akifanya mapenzi na mwanafunzi katika maabara ya shule hiyo amesimamishwa kazi
akisubiri hatua za kinidhamu dhidi yake.
Ofisa Elimu wa
Wilaya, Christopher Sinkamba akizungumza alisema kwamba maamuzi hayo
yamechukuliwa baada ya wananchi wengi kulalamika.
Sinkamba alisema mwalimu anayehusika
ametambuliwa kama Raphael Mwape na kwamba sasa anasubiri hatua za kinidhamu
dhidi yake.
Alisema kwamba
utawala wa shule ulifikisha suala hilo Polisi lakini walishindwa kumshtaki kwa
tuhuma za kubaka kwa kuwa binti huyo ni zaidi ya miaka 16.
Na wakati alipoulizwa swali kwanini
mwanafunzi huyo wa kike ametimuliwa shule, ofisa huyo alisema kwamba
hawajamfukuza lakini walilazimika kumhamisha shule kutokana na sheria za shule
hiyo.
Ilielezwa kuwa
tukio hilo lilifanyika saa 12 jioni ambapo Mwape alionwa na mabinti wengine
wawili wa shule hiyo akifanya mapenzi na binti huyo katika maabara B ya shule
hiyo. Mwanafunzi huyo alisema kwamba hiyo haikuwa mara ya kwanza kwa mwalimu
huyo kumuingilia na kwamba siku hiyo alilazimika kufanya hivyo baada ya
kushinikizwa na mwalimu aliyemuita wakati akirejea bwenini.
Alisema pamoja na kukataa kwake
alimshinikiza kwa kudai kuwa alikuwa amemgharamia sana.Mwalimu huyo ana mke.
0 comments:
Post a Comment