Waumini
wawili wa Kanisa Siloam wamekufa maji wakibatizwa katika Mto Ungwasi wilayani
Rombo baada ya mmoja wao kupandisha mapepo na kuwatumbukiza majini wenzake.
Mkuu
wa Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro Agnes Hokororo, amethibitisha tukio hilo
lililotokea jana saa sita mchana.
Ubatizo
huo ulifanyika kwenye kina kirefu cha mto huo.
Amesema
wakati ibada ya ubatizo mmoja wa waumini aliyepandisha mapepo alimtumbukiza
mmoja wa watu waliokuwa wakisubiri kubatizwa na mchungaji.
Hokororo
amesema muumini mmoja alipoona mwenzake ametumbukizwa majini aliamua kumwokoa,
ndipo aliyepandisha pepo alipowashikilia wote wawili ndani ya maji na
kuwasababishia kifo.
Amesema
watu watatu akiwamo mchungaji wa kanisa hilo lililopo katika Kijiji cha
Mandechini wanashikiliwa.
0 comments:
Post a Comment