Mgombea
wa urais katika muungano wa NASA nchini Kenya Raila Odinga amewataka wafuasi
wake kutoshiriki tendo la ndoa mkesha wa siku ya uchaguzi.
Bwana Odinga amefananisha
uchaguzi huo na vita akisema kuwa kushiriki ngono kabla ya kwenda vitani ni
mkosi mbaya ambao unaweza kusababisha mtu kushindwa.
''Tunaenda vitani na lazima
tuhifadhi nguvu yetu kabla ya siku ya vita ambayo ni Agosti 8'', alisema mjini
Homabay eneo la magahribi mwa Kenya.
''Hakuna hata mmoja wetu ambaye
anafaa kushiriki ngono kabla ya mkesha wa siku ya uchaguzi'.
Odinga hususan aliwasisitizia
wanaume akisema itasababisha wengine wao kutopiga kura.
Wanawake alisema ,hawafai
kukubali kushiriki katika tendo la ndoa na waume zao usiku wa kuamkia siku ya
uchaguzi, alisema.
''Kila mwanamke anafaa kumnyima
mumewe haki yake ya tendo la ndoa'' ,alisema.
''Hatua hiyo itatufanya kuamka mapema alfajiri ili kupiga
kura na kulinda kura na kuilinda siku nzima hadi pale kura zitahesabiwa na
kutangazwa'.
Sio mara ya kwanza kwa kiongozi
huyo wa chama cha ODM kukataza tendo la ngono wakati wa uchaguzi.
Wakati wa uzinduzi rasmi wa
kampeni za muungano wa NASA mjini Kakamega magharibi mwa Kenya , tarehe 3 mwezi
Juni, Odinga aliwaambia wafuasi wake kusubiri hadi pale matokeo
yatakapotangazwa ili kuweza kufurahia tendo hilo la ndoa.
''Nawaomba wanawake, kuwaambia
waume zao kusubiri hadi baada ya uchaguzi ili kuweza kushiriki tendo hilo ili
kusherehekea ushindi wetu''.
0 comments:
Post a Comment