Tuesday 18 July 2017

KISIWA CHASHINDA SHINDANO LA UKWEAJI MNAZI

Kisiwa cha Cook ndio bingwa duniani wa shindano la ukweaji minazi imeripotiwa.

George Iona aliibuka mshindi katika shindano lillilokuwa na wawaniaji 16,akishinda kwa uchache kulingana na idhaa ya redio ya Tahiti.
Aliupanda mti huo wenye urefu wa mita nane kwa sekunde 5.62 katika shindano hilo lililofanyika katika eneo la kumbukumbu la Tahiti.
Alikuwa mbele ya Fiapai Ellio wa Samoa ya Marekani mtu aliyepigiwa upato kushinda.
Lengo la shindano hilo jipya ,ni kupanda mti huo haraka iwezekanavyo huku kila mpandaji akipewa fursa mbili za kuweka muda bora zaidi.
Hatua hiyo inashirikisha kuvaa kamba katika visigino vya miguu ili kusaidia kukwea kwa garaka.
Akizungumza na idhaa ya redio ya Tahiti 1, mwaandalizi Enoch Laughlin amesema kuwa ushindi mkubwa wa bwana Iona uliwashangaza watu wengi, kwa kuwa kila mtu alitarajia kwamba mwanariadha wa Samoa ataibuka mshindi kufuatia ushindi wao katika mashindano ya awali.

Mshindi huyo aliwaambia maripota kwamba ni fahari kubwa na furaha kushinda taji hilo.

0 comments:

Post a Comment