Mshambuliaji
mpya wa Everton Wayne Rooney, amekuwa kivutio wakati msafara wa timu hiyo
ulipowasili jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Everton
iliyowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa (JNIA) ilipokelewa na Waziri wa
Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk Harrison Mwakyembe.
Ndege
binafsi ya Everton iliwasili katika uwanja huo majira ya saa 2:39 Asubuhi,kabla
ya wachezaji kuanza kuingia kwenye basi lao maalumu, huku wakipitia kwa Waziri
Mwakyembe na kumpa mkono.
Wakati
wachezaji wa Everton wakiingia kwenye basi, mashabiki waliokuwa nyuma ya geti
la kuingilia VIP kila mmoja alionyesha shauku ya kumuona mubashara 'live'
Rooney ,ambaye kana kwamba msafara huo ulilitambua hilo na Rooney kuwa wa
mwisho kushuka.
Aliposhuka
Rooney alikwenda kumpa mkono Waziri Mwakyembe na kisha kuelekea kwenye basi
maalumu la timu hiyo, wakati akielekea kwenye basi baadhi ya mashabiki wake
waliokuwa uwanjani hapo walianza kupaza sauti wengine wakitaka ageuke asimame
na kupunga mkono.
Everton itacheza mechi ya kirafiki ya kimataifa
kesho kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam dhidi ya Gor Mahia ya Kenya.
0 comments:
Post a Comment