Ajuza
wa miaka 86 anayejulikana sana kwa wizi wa vito tangu miaka ya 50 ameshtakiwa
kwa wizi.
Doris Payne alikamatwa katika
duka moja katika eneo la Chamblee mjini Georgia kwa wizi wa vito vyenye thamani
ya dola 86 kulingana na maafisa wa polisi.
Ameachiliwa kwa dhamana.
Alipatikana amevalia kifaa cha
kumfuatilia mtu mguuni katika shtaka jingine la wizi wa dukani.
Payne amehudumia vifungo kadhaa
kwa uhalifu aliotekeleza.
Anadaiwa kuiba vito vyenye
thamani ya dola milioni 2 na akaangaziwa katika makala ya 2013.
Mfanyikazi mmoja wa duka alisema
kuwa aliiba vitu kadhaa kutoka kwa duka la dawa , vifaa vya kielektroniki na
katika duka la mboga.
Wakili wake Drew Finding
alinukuliwa na chombo kimoja cha habari akisema: Hiki ni kisa cha kipekee
ikilinganishwa na visa vyengine vilivyopita.
Tunazungumzia kile bibi wa miaka
86 anachotaka ili kuweza kuishi kila siku, ikiwemo chakula na matibabu.
Hivi karibuni alikiri kuiba mkufu
kutika duka moja huko Atlanta.
Alihukumiwa kifungo cha nyumbani
na kupigwa marufuku kuingia katika maduka ya jumla katika eneo hilo.
0 comments:
Post a Comment