Mkosoaji mashuhuri wa rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, atapewa ulinzi wa
polisi baada ya kupokea vitisho vya kuuliwa.
Bunge na polisi
walifanya uchunguzi na kubaini kuwa kuna vitisho vya kuuliwa dhidi ya Makhosi
Khoza ambaye ni mbunge wa chama cha ANC.
Bi Khoza amemtaka
Bwana Zuma aondoke madarakani akimtaja kuwa kiongozi wa kuchukiza ambaye
amekumbwa na madai ya ufisadi.
Zuma anakana kufanya
lolote baya na hakuna madai kuwa amehusishwa na vitisho hivyo.
0 comments:
Post a Comment