Kampuni ya mawasiliano ya Samsung imeanza kuuza simu
nyingine ambazo inasema imetumia baadhi ya sehemu na vipande vilivyokuwa kwenye
simu za Galaxy Note 7 ambazo zilikumbwa na matatizo.
Simu hizo za
Galaxy Note 7 zilikuwa zinashika moto na kulipuka kutokana na tatizo kwenye
betri zake.
Kampuni hiyo
imesema simu hizo mpya kwa Kiingereza Note Fan Edition zitapunguza athari za
kimazingira kutoka kwa mabaki ya simu hizo ambazo ziliacha kuuzwa kutokana na
hitilafu hizo.
Simu hizo mpya
zitauzwa Korea Kusini pekee na zitaanza kuuzwa tarehe 7 Julai.
Kampuni hiyo
imesema simu hizo zitakuwa na betri ndogo ambazo ni salama zaidi kuliko simu
hizo za awali.
Samsung iliacha kuunda simu za Galaxy
Note 7, ambayo ilifaa kuisaidia kampuni hiyo kushindana na simu mpya za iPhone,
mwishoni mwa mwaka jana baada ya kwanza kuwaomba wateja wazirejeshe nzifanyiwe
ukarabati lakini hatua hiyo ikakosa kufaulu.
Inakadiriwa
kwamba simu 2.5 milioni zilirejeshwa kwa kampuni hiyo.
Simu hiyo mpya
itakwua na vipande kutoka kwa simu ambazo zilirejeshwa na wateja na vipande
vingine kutoka kwa simu za Samsung ambazo hazikuwa zimeuzwa.
Betri ndogo na bei nafuu
Watetezi wa
mazingira wamekuwa wakiishinikiza Samsung kutumia tena baadhi ya sehemu za
Galaxy Note 7 ili kupunguza taka ambazo zingetokana na simu hizo.
Inakadiriwa kwamba
simu 400,000 mpya zitaanza kuuzwa kuanzia Ijumaa.
Bei yake itakuwa ni
won 700,000 za Korea ($615; £472), ambayo ni 30% chini ya bei iliyokuwa ya
Galaxy Note 7.
Simu hizo zitakuwa na
betri za 3,200 mAh na Samsung wanasema betri hizo zimechunguzwa vyema.
Note 7 zilitumia betri
za nguvu ya 3,500 mAh.
Simu za Samsung Galaxy
Note 8, ambazo zitatolewa kuifuata Note 7, zinatarajiwa kuanza kuuzwa baadaye
mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment