Polisi nchini
China wamewakamata wanachama 18 wa dhehebu lililopigwa marufukua.
Baadhi ya wanachama wa kundi hilo ni maarufu kwa kumpiga
mwanamke hadi kufa kwenye duka la McDonald mwaka 2014, baada ya mwanamke huyo
kukataaa kuwapa namba yake ya simu.
Dhehebu hilo linalofahamika kama Church of Almighty God
lilianzishwa miaka ya 1990 na linadai kuwa Yesu alirudi duniani kama mwanamke
nchini China.
Serikali ya China mara kwa mara huvamia madhehebu na
kuwakamata wanachama wengi kwa miaka kadhaa.
Wakati wa
kuwakamata polisi pia walichukua komputa na vitabu vinavyotumiwa na dhehebu
hilo.
Imani ya dhehebu hilo ni kuwa Yesu alirudi duniani kama
mwanamke.
Mtu pekee anayedai kuwasiliana na mwanamke huyo ni mwalimu wa
zamani Zhao Weishan, ambaye alilianzisha miaka 25 iliyopita na sasa ametorokea
Marekani.
0 comments:
Post a Comment