Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa ripoti mpya kuhusu hali ya
afya ya uzazi likieleza kuwa ngono kwa njia ya mdomo imeendelea kuwa tishio
kubwa kwa usambazaji wa magonjwa ya zinaa na kupelekea hata kutotibika.
Uchambuzi wa WHO umeeleza
kuwa taarifa zilizokusanywa katika nchi 77 duniani zimeonesha kuwa magonjwa ya
zinaa ya gonorrhea yaliyoambukizwa kwa kushiriki ngono kwa midomo (oral sex)
yamekuwa yakipambana vikali na dawa kusambaa kwa haraka zaidi.
Dk. Teodora Wi, wa
WHO ameeleza kuwa kumekuwa na kesi tofauti katika nchi za Japan, Ufaransa
na Uhispania ambapo maambukizi ya magonjwa hayo ya zinaa yamekuwa hayawezi tena
kutibika.
Ameeleza kuwa aina hiyo ya
ngono inasambaza kwa kasi bakteria wa magonjwa hayo ya zinaa na kwamba upungufu
wa kondom katika nchi kadhaa pia umesaidia katika usambazaji huo.
Mtaalam huyo wa WHO amesema
kuwa utafiti huo umeonesha kuwa takribani watu milioni 78 duniani kote hupata
maambukizi ya magonjwa ya zinaa kila mwaka, na kwamba dawa za kupambana na
magonjwa hayo zimekuwa zikizidiwa nguvu.
“Gonorrhea ni mdudu mjanja
sana, kila tunapozindua aina fulani ya tiba kuitibu, mdudu anazidi kuongeza
nguvu za kuishinda tiba hiyo,” BBC inamkariri Dk. Teodora Wi.
Alisema kuwa kwa bahati
mbaya maambukizi mengi ya gonorrhea yako kwenye nchi zinazoendelea ambapo ni
ngumu zaidi kubaini dalili za ugonjwa kwa haraka.
0 comments:
Post a Comment