Monday 10 July 2017

KUNYWENI KAHAWA INA FAIDA LUKUKI……..

Dhana potofu kuwa unywaji kahawa unaleta shinikizo la damu, umesababisha kinywaji hicho kutumika kwa asilimia 10 tu nchini.

Akizungumza katika Banda la Bodi ya Kahawa Tanzania lililopo katika viwanja vya Maonyesho ya Kimataifa ya 41 (Sabasaba), Ofisa Uhamasishaji wa bodi hiyo, Frank Mlay amesema dhana hiyo imesababisha zao hilo likose thamani hapa nchini.

Badala yake, Mlay amesema kinywaji cha zao hilo kina faida nyingi za kiafya ikiwa ni pamoja na kuzuia saratani, ugonjwa wa kutetemeka (Parkinson Disease) na maumivu ya ngozi.

Amesema asilimia 90 ya kahawa inasafirishwa nje ya nchi na asilimia 10 pekee ndiyo inayotumika hapa nchini.

Meneja masoko na ubora wa bodi hiyo, Rogalus Meela amesema kama Watanzania wataitumia kahawa ipasavyo wataiongezea mnyororo wa thamani ambapo akija mnunuzi kutoka nje atalazimika kuinunua kwa bei ya juu.

0 comments:

Post a Comment