Mtandao wa
kutuma ujumbe kwa njia ya simu wa Telegram, umeahidi kuwa utafunga akaunti
zinazohusiana na ugaidi, baada ya serikali ya Indonesia kufunga huduma za
mtandao huo nchini humo.
Wizara ya mawasialiano na teknolojia nchini Indonesia,
ilifunga huduma za Telegram siku ya Ijumaa na kutishia kufunga mifumo yake
yote.
Indonesia inadai kuwa Telegram imetumiwa kuunga mkono itikadi
kali na kutoa maelekezo ya kufanya mashambulizi.
Mwanzilishi wa mtandao huo amesema kuwa, ameghadhabishwa na
hatua hiyo.
Katika taarifa
Pavel Durov alisema kuwa, Telegram sasa imeondoa akaunti zote zinazohusika na
ugaidi zilizotajwa na serikali.
Hatua ya serikali inakuja huku kukiwa na wasi wasi wa kuibuka
kwa kundi la Islamic State kusini mashariki mwa Asia.
Kundi hilo limedai kuhusika kwenye mashambulizi kadha nchini
Indonesia mwaka huu na limepigana na jeshi mjini Marawi katika kisiwa cha mindanao
nchini Ufilipino.
0 comments:
Post a Comment