Mhadhiri
wa Chuo Kikuu cha Aga Khan Eunice Pallangyo, amefanya utafiti na kubaini kwamba
vituo vya afya havitoi huduma ya uangalizi kwa kinamama baada ya kujifungua
hali inayosababisha vifo vya
uzazi kuongezeka.
Ripoti
ya Jamii na afya DHS ya ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa mwaka 2015/16 inaonyesha
kuwa, kuna vifo 556 vya uzazi katika kila vizazi hai laki 1, wakati kulikuwa na
vifo mia 4 na 54 katika kila kila vizazi hai laki 1 mwaka 2010/11.
Akizungumzia
utafiti huo mbele ya wadau wa afya wa wilaya ya Ilala, Pallangyo amesema katika
vituo vya afya 27 alivyotembelea, hakuna huduma ya uangalizi wa kinamama baada
ya kujifungua.
Amesema
mwongozo wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
unaelekeza kuwa baada ya wajawazito kujifungua wanatakiwa kuwa katika uangalizi
katika kipindi cha siku 42.
Kwa
mujibu wa mwongozo huo, mwanamke baada kujifungua anatakiwa kufanyiwa uchunguzi
ndani ya saa 24 baada ya kujifungua.
Ameshauri
Serikali kusimamia utekelezaji wa miongozo inayoweka kwa kuzungumza na
watendaji, ili kufahamu changamoto zinazowakabili.
Mkurugenzi
wa Huduma za Uuguzi na Ukunga wa Wizara ya Afya Gustan Moyo, amesema Serikali
imekuwa ikiboresha huduma za afya.
0 comments:
Post a Comment