Awali watuhumiwa hao walipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma ya uhujumu uchumi na kula njama, kughushi, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kuisababisha hasara serikali, lakini watuhumiwa hao leo tena wamepandishwa kizimbani na kuongezewa makosa mengine sita ya ya utakatishaji wa fedha na kufikisha jumla ya mashtaka 12.
Mbali na
hilo watuhumiwa hao wamekwama baada ya kukosa dhamana tena na wote
wamerudishwa rumande mpaka tarehe 14 Juni mwaka huu ambapo kesi yao itasomwa
tena katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment