Betri kubwa zaidi ya lithium duniani itaundwa na kuwekwa nchini
Australia, kupitia makubaliano kati ya kampuni inayounda magari ya kutumia umeme
ya Tesla na kampuni ya kawi ya Australia Neoen.
Betri hiyo inatarajiwa
kulikinga jimbo la Australia Kusini dhidi ya mgogoro wa kawi sawa na
uliosababisha kukatizwa kwa umeme kabisa katika jimbo hilo Septemba 2016 baada
ya kutokea kwa tufani mbaya zaidi katika kipindi cha miaka 50, waziri mkuu wa
jimbo hilo Jay Weatherill.
Watu zaidi ya 1.7
milioni huishi katika jimbo hilo ambalo ni kubwa mara 40% zaidi ya jimbo la
Texas. Jimbo hilo lina ukubwa wa zaidi ya kilomita mraba 980,000 (maili mraba
380,000).
Mkuu wa kampuni ya
Elon Musk amethibitisha kwamba kampuni hiyo itaunda betri hiyo katika kipindi
cha siku 100, na ikishindwa kufanya hivyo basi itaunda betri hiyo bila malipo.
Betri hiyo itakuwa na
uwezo wa megawati 100 (megawati 129 kwa saa), na inatarajiwa kuanza kutumiwa
mwaka huu.
"Bila shaka kuna
changamoto kadha, kwa sababu itakuwa betri kubwa zaidi duniani kwa mbali,"
Musk alisema akiwa Adelaide Ijumaa.
Aliongeza kuwa
"betri inayoifuata hiyo kwa ukubwa ina uwezo wa megawati 30".
Betri hiyo mpya ya
Tesla, ambao wameshirikiana na kampuni ya nishati ya upepo ya Neoen, itakuwa
ikifanya kazi bila kuzimwa na itatoa umeme zaidi hasa wakati wa dharura.
"Itakabilisha
kabisa jinsi kawi mbadala inavyohifadhiwa, na pia kuimarisha mfumo wa kusambaza
umeme wa jimbo la Australia Kusini Weatherill alisema.
Siku 100 alizoahidi
Musk zitaanza kuhesabbiwa baada ya mkataba kutiwa saini rasmi.
Tesla wamekuwa
wakipanua biashara yao ya uundaji wa betri sawa na uundaji wa magari ya umeme.
0 comments:
Post a Comment