Kaburi
la Mtunzi wa Wimbo wa Taifa wa Uganda marehemu George Kakoma limefukuliwa na
watu wasio julikana, huku kukiwa na wasiwasi kwamba mabaki ya mwili wake
yameibiwa.
Gazeti la Daily Monitor la
Uganda, limechapisha picha ya kile kilichoonekana kuchimbuliwa kaburi hilo na
kuharibiwa.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, polisi
wa eneo hilo na mjane wa marehemu wameomba kibali mahakamani kuweza kuchimbua
kaburi hilo, ili kuweza kuthibitisha kama mabaki yake yapo ama yameondolewa.
Marehemu Kakoma alifariki dunia
miaka mitano iliyopita.
0 comments:
Post a Comment