Monday 17 July 2017

WAZIRI ALAUMIWA KWA KUTUMIA DOLA 770,000 KWA MAUA NA ZAWADI……

Lindiwe Sisulu
Chama kiku cha upinzani nchini Afrika Kusini cha Democratic Alliance (DA) kimetaka kuelezwa na waziri wa nyumba Lindiwe Sisulu, jinsi idara yake ilitumia dola 770,000 kwa maua na zawadi zingine wakati wa kipindi cha bajeti cha mwaka 2013/2014.


Utata unaibuka wakati Bi Sisulu, binti wa mpinzani mkubwa wa utawala wa ubaguzi wa rangi Walter Siusulu, anakabaliana na wapinzani wengine kuchukua nafasi ya Rais Jacob Zuma, kama kiongozi wa chama tawala cha ANC.
Bi Sisulu alifichua matumizi hayo akijibu swali la bunge, na sasa chama cha DA kinataka orodha yote ya watu walionufaika kutokana na pesa hizo.
"Pesa hizo zingetumiwa kujenga nyumba 100 za gharama ya nchini na kusaidia kukabiliana na suala la ukosefu wa nyumba nchini Afrika Kusini," chama hicho kilisema.
Bi Sisulu hajazungumza chochote kuhusu taarifa hiyo ya DA.
Siku ya Jumamosi alitoa wito kwa wafuasi wake kufanya kampeni ya kuchaguliwa kwake kwa maadili mema na kuapa kupambana na ufisadi.


Mshindi anatarajiwa kuwa mgombea wa uara wa chama mwaka 2019.

0 comments:

Post a Comment