Tundu
Lissu na Kituo cha Haki za Binadamu zimeungana kwa pamoja katika kupinga
kitendo cha kuvamiwa na kulipuliwa Ofisi za IMMMA Advocates.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC),
kimemtaka Kaimu Jaji Mkuu, Ibrahim Juma kukemea hadharani shambulizi
lililofanyika katika ofisi za wanasheria za Immma Advocates.
Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen KijoBisimba amesema
tangu kutokea mlipuko usiku wa kuamkia Agosti 26, hakuna kiongozi wa Serikali
ambaye amekemea.
Amesema hata kaimu jaji mkuu anayesimamia mhimili wa
Mahakama naye amekaa kimya kama vile hakuna tukio lililotokea.
Dk KijoBisimba amesema leo Agosti 29 kuwa, kitendo
cha mawakili kuvamiwa kimewatia hofu wanataaluma hao.
0 comments:
Post a Comment