Waalimu wawili waliokuwa wakifanya mazoezi kwa vitendo katika shule
ya sekondari ya Kikala wilayani Lushoto mkoani Tanga, wanashikiliwa na Jeshi la
Polisi kwa kosa la kufanya mapenzi na wanafunzi wawili wa kidato cha tatu
shuleni hapo.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa
Wilaya ya Lushoto January Lugangika, ambapo amesema kuwa waalimu wa wanafunzi
hao wamekiuka maadili ya ualimu, na kwamba watachukuliwa hatua zaidi huku
akiongeza kuwa tabia kama hizo zinaleta kichefu chefu kwa jamii.
Amewataka wazazi kuwafatilia
watoto wao kwa kila hatua, wajue wanafanya nini shuleni na kama mzazi hamfatilii
anaweza kufanya mambo usiyoyajua na badala yake ukashtukia ana mimba ya miezi
hata sita.
Hata hivyo kwa upande wa Afisa Elimu wa Sekondari Wilaya ya Lushoto
Kassim Singato, amesema endapo kutakuwa na masomo ya ziada ni lazima yafahamike
muda yanapoisha ili wazazi waweze kufuatilia mwenendo wa watoto wao.
0 comments:
Post a Comment