Serikali
imewataka watoa huduma za afya katika kituo cha afya cha Matai kilichopo
Wilayani Kalambo kutoa huduma bora kwa wanawake wajawazito.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani
hapo ya kutembelea hospitali hiyo pamoja na kuongea na watumishi wa sekta ya
afya kujua changamoto zinazowakabili
Amesema kuwa wajawazito wanapaswa kupata huduma bora kila
wanapofika kliniki kila mwezi kwa kuangaliwa mfano dalili za kifafa cha mimba,
wigi wa proteini pamoja na vihatarishi vingine vinavyoweza kusababisha
uzazi pingamizi hivyo kupelekea vifo kwa mama au mtoto wakatiwa kujifungua
“Nawapongeza sana kwa kutenga dirisha la wazee
ila kusiwepo tu dirisha bali muwape dawa wazee wasio kuwa na uwezo,hivyo kama
kuwakatia mfuko wa bima ya jamii (CHF)ni gharama basi wapatieni vitambulisho
vya matibabu bure ili wazee wakija kwenye matibabu wasije na barua za watendaji
wa vijiji”
Hata
hivyo, Kwa upande wa madawa Ummy amesema kuwaa hakuna masharti magumu ya
ununuzi wa madawa na vifaa tiba kwa kutumia pesa za CHF
0 comments:
Post a Comment