Mgini Aron 37 mkazi wa Magunga Wilaya ya Butiama Mkoani
Mara, amefariki dunia baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali na mkewe Jeni
Mwenda 25, kwa sababu ya wivu wa mapenzi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mara Jafari Mohamed, amesema tukio hilo lilitokea Julai 30
majira ya saa 11:15 jioni katika kitongoji cha Kitaramanka Kata ya Mirwa.
Amesema baada ya marehemu kutoka matembezini alifika
nyumbani moja kwa moja na kuingia bafuni, kitendo kilichomkasirisha mkewe
akidai kwanini amerudi na kuingia bafuni moja kwa moja.
Kamanda Mohamed amesema baada ya marehemu kuambiwa hivyo
walianza ugomvi na mpenzi wake huyo, katika purukushani ndipo Jeni alipomchoma
na kitu chenye ncha kali upande wa titi la kushoto na kusababisha kifo chake.
Kamanda amesema mtuhumiwa ameshakamatwa na Jeshi la
Polisi kwa ajili ya mahojiano na uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha
kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara kwa uchunguzi zaidi.
0 comments:
Post a Comment