Wakati
ugonjwa wa kipindupindu ukiendelea kuwatesa wananchi wa Wilaya ya Mbarali
mkoani hapa, ugonjwa huo umepiga hodi ndani ya jiji la Mbeya na hadi leo
Alhamisi wagonjwa watano waligundulika.
Meya
wa jiji hilo, Mchungaji David Mwashilindi amebainisha hilo leo kabla ya kuanza
kwa kikao cha Baraza la Madiwani la jiji hilo la linaloketi kwa ajili ya
kupitia taarifa mbalimbali za mwaka wa 2016/2017.
Meya
Mwashilindi alisema tayari ugonjwa upo kwenye kata za Iyela, Ilemi na Iganjo na
wagonjwa hao wametoka katika kata hizo, hivyo aliwataka madiwani kuhakikisha
wanatoa ushirikiano kwa wataalamu na wananchi kudhibiti ugonjwa huo.
“Ndugu zangu tayari ugonjwa huu umeingia ndani
ya jiji letu na wagonjwa watano wamegundulika kupata kipindupindu.
Hivyo
basi ninaona madiwani tuhakikishe tunatoa kila aina ya ushirikiano kwa
wataalamu wetu wanaofika kwenye maeneo yenu kuchukua hatua mbalimbali dhidi ya
ugonjwa huu kwa wananchi,” alisema meya huyo.
0 comments:
Post a Comment