Bibi harusi katika jimbo la Tennessee
nchini Marekani, ametiwa nguvuni baada ya polisi kusema kuwa alitoa bunduki
kwenye gauni lake la harusi na kumtishia mumewe saa chache tu baada ya kufunga
ndoa.
Kate
Elizabeth Prichard mwenye umri wamiaka 25, alikuwa bado amevalia gauni la
harusi wakati alipokamatwa katika hoteli moja katika mji wa Murfreesboro.
Alidaiwa
kuchukua bunduki aina ya pistol na kuiweka kwenye kichwa cha mumewe na
kufyatua.
Bunduki
haikuwa na risasi lakini baadae alidaiwa kuijaza risasi na kufyatua angani,
jambo lililowafanya waliokuwa wakishuhudia tukio hilo kukimbia.
Walioshuhudia tukio
hilo walitoa taarifa kwa polisi ndipo polisi walipowasili eneo la tukio.
Walisema
wawili hao walikuwa wakinywa pombe nje ya hoteli.
Sajenti
polisi katika mji wa Murfreesboro Kyle Evans amesema kuwa maharusi hao wote
wawili hawakutoa ushirikiano kwa mamlaka husika juu ya tukio nhilo.
Sajenti
Evans amesema kuwa bibi harusi alijaribu kuficha silaha bafuni katika hoteli
walimokuwa.
0 comments:
Post a Comment