Mlipuko wa Homa ya Nguruwe ulioikumba India umesababisha vifo vya
watu 1,094, kwa kipindi cha miezi minane iliyopita huku ikisemekana kuwa
ugonjwa huo ni hatari zaidi na unasambaa kwa kasi.
Idadi ya watu waliofariki kwa mwaka huu ni mara nne zaidi ya idadi
iliyoripotiwa katika kipindi sawa na hicho mwaka 2016, ambapo maambukizi ya
ugonjwa huo yalikuwa yameshuka sana.
Aidha katika Jimbo la Maharashtra lililopo magharibi mwa nchi hiyo,
ndilo lililoathirika zaidi ambapo waliofarikini kutokana na ugonjwa huo ni
takribani watu 437 kwa mujibu wa takwimu za wizara ya afya nchini humo.
Hata hivyo Mlipuko mbaya zaidi wa homa hiyo ambao uliikumba nchi hiyo
ulitokea miaka ya 2009-2010, ambapo watu 50,000 waliambukizwa na wengine 2,700
kufariki dunia nchini humo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Matibabu katika hospitali ya Shanthi
ambayo ni ya binafsi Dkt Sanjay Gururaj, amesema kuwa si lazima kwa hospitali
za binafsi kutoa ripoti ya hali ya maambukizi ya ugonjwa huo Serikalini.
0 comments:
Post a Comment