Mamlaka katika Mji wa New Delhi,
India zimearifu kuwa zimewakamata Wanawake wawili wa
Kiafrika baada ya kuwakuta na Dawa za Kulevya aina ya cocaine yenye thamani ya
Dollar Milioni 6 za Marekani.
Katika taarifa
zilizochapishwa na DNA INDIA zimesema Narcotics Control Bureau (NCB) imemkamata
mwanamke Mtanzania sanjari na Mnigeria wakati wanabadilishana dawa hizo katika
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Indira Gandhi, Delhi Jumatano August 16, 2017.
Kwa mujibu wa
Maafisa wa NCB,kufuatia upelelezi uliofanywa, walifanikiwa kumkamata Mtanzania
huyo aliyetambulika kwa jina la Beatrice Kemmy Ndyetabula ambaye ana umri wa
miaka 40, mara tu alipowasili kwa Ndege ya Go Air flight akitokea Mumbai.
Afisa Mkuu wa NCB
alisema:>>>”Alikuwa
amebeba mabegi mawili. Ilikuwa wakati wa kukaguliwa ndipo zilibainika 4 kg za
cocaine zikifungwa kwenye vifungashio 27. Alisema kwamba aliwasili Mumbai
akitokea Kenya kisha akasafiri hadi Delhi kuukabidhi mzigo huo kwa muhusika.”
Maafisa hao walisema
baada ya kumhoji, mwanaume ambaye alikuwa amkabidhi mzigo huo ambaye
anafahamika kwa jina la Augustin, naye alikamatwa.
0 comments:
Post a Comment