Kampuni kubwa zaidi ya mitandao ya
kijamii duniani Facebook, inatarajia kuanza kutoa huduma ya video itakayokuwa
ikiitwa ”watch” ama tazama.
Facebook inasema kwamba imewekeza
mamilioni ya dola katika kuufanya mfumo huo kupendwa zaidi.
Teknolojia
hiyo imebuniwa ili kushindana na televisheni za kawaida pamoja na mitandao ya
you tube Netflix, twitter na snap chat.
Facebook
inasema kwamba imewekeza mamilioni ya dola katika kuifanya huduma hiyo kupendwa
zaidi.
Nayo Kampuni
ya Disney jana ilitangaza kuwa kuanzia mwaka 2019, itafuta makubaliano kati
yake na kampuni ya Neflix na kuunda huduma yake mpya ya video.
Facebook
tayari ina vipindi kadha vikiwemo vya michezo, vya familia na vya televisheni
ya National Geographic.
Watch itaanza
kuonyeshwa nchini Marekani kabla ya maeneo mengine kuruhisiwa kutazama.
0 comments:
Post a Comment