Mahakama
ya juu nchini India imeamua kuwa talaka ya mara moja katika dini ya kiislamu ni
kinyume na katiba, uamuzi ambao umekuwa ni ushindi mkubwa kwa haki wanawake.
India ni moja ya nchi chache ambapo
mwanamume muislamu anaweza kumtaliki mkewe kwa kutamka neno talaq mata tatu.
Uamuzi huo wa mahakama unafutia kesi
zilizokuwa zikipinga talaka hiyo.
Kesi hizo ziliwasilishwa mahakamani
na wanawake watano waislamu, waliokuwa wamepewa talaka kwa njia hiyo pamoja na
na makundi mawili ya kutea haki.
Miaka ya hivi karibuni visa vingi
vimeibuka ambapo wanaume waislamu huwataliki wake zao kwa kutamka neno talaq
mara tatu, kwa njia ya simu au kwa kutuma ujumbe ya sms, kupitia WhatsApp na
Skype.
Licha ya njia hiyi ya kutaliki
kutumiwa kwa miongo kadha, hiajatajwa popote pale kwenye Sharia au Koran.
0 comments:
Post a Comment