Wednesday 16 August 2017

MKAPA MIONGONI MWA WAATHIRIWA WA UPANUZI WA BARABARA...

Nyumba inayoaminika kumilikiwa na mke wa aliyekuwa rais wa zamani wa Tanzania Benjamini Mkapa itavunjwa ili kuruhusu upanuzi wa barabara ya Morogoro.

Nyumba hiuyo ya Anne Mkapa itakuwa miongoni mwa maelfu ya nyumba, ambazo zinatarajiwa kuvunjwa shughuli itakayowaathiri zaidi ya watu 10,000.
Gazeti la Th Citizen lilitembelea nyumba hiyo inayodaiwa kumilikiwa na bi Anne na mwanamke mmoja aliyepatikana katika eneo hilo alithibitisha kwamba ni nyumba ya Mkapa.

Natoka familia ya Mkapa, lakini siwezi kusema mengi kuhusu swala hili,iwapo munataka maelezo zaidi ni muhimu kuwasiliana naye, alisema mwanamke huyo.

0 comments:

Post a Comment