Serikali ya Misri imewakamata madaktari ambao wanatuhumiwa kuhusika
na mtandao wa biashara ya kuuza viungo vya binadamu.
Jeshi la polisi nchini humo
juzi lilivamia katika kituo kimoja maarufu cha afya kinachojihusisha na
matibabu ya ini na kuwakamata madaktari kadhaa pamoja na wafanyakazi wengine wa
kituo hicho.
Madaktari hao wanatuhumiwa
kuondoa viungo vya binadamu kwa wananchi masikini wanaofika katika kituo hicho
ikiwa ni pamoja na wakimbizi na kuwauzia wananchi matajiri na watu wa nchi za
nje wenye ukwasi mkubwa.
Miaka saba iliyopita, Shirika
la Afya Duniani (WHO) liliitaja Misri kama nchi ya tano kati ya nchi
zinazoongoza kwa kufanya biashara ya viungo vya binadamu duniani kote.
Taarifa hiyo ilisababisha Serikali ya Misri kuweka sheria kali dhidi
ya wanaojihusisha na biashara hiyo.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, uchunguzi na oparesheni
maalum inayoongozwa na Wizara ya Afya ya nchi hiyo inalenga hospitali binafsi
na vituo vya afya vyenye leseni na visivyokuwa na leseni.
0 comments:
Post a Comment