Instagram
imegundua dosari katika mfumo wake iliofichua nambari za simu za watu maarufu
pamoja na anwani zao kwa wadukuzi wa mitandao.
Mtandao
huo unaomilikiwa na Facebook tayari umewasiliana na watu hao ili kuwaelezea
dosari iliotokea.
Imesema
inaamini kwamba wadukuzi waliwalenga watu maarufu ili kupata habari zao za
mawasiliano.
Instagram
imesema kuwa nywila hazikuibiwa lakini ikawaonya wateja wake kuchunguza
mienendo isiokuwa ya kawaida katika akaunti zao.
Hatahivyo
haikutaja ni akaunti za watu gani zilizoathirika.
Dosari
hiyo ya kiusalama wa mitandao ilitokea kutokana na tatizo katika programu ya
kampuni hiyo.
Hatahivyo
imesema kuwa tatizo hilo limeangaziwa.
Kampuni
hiyo imewaonya wateja wake kuwa waangalifu kuhusu simu wasizotarajia, ujumbe na
barua pepe.
Instagram
ina zaidi ya wateja milioni 500 duniani,wateja milioni 300 wanautumia mtandao
huo mara moja kwa siku.
0 comments:
Post a Comment