Hofu
imekumba kijiji cha Shayamoya katika jimbo la KwaZulu Natal nchini Afrika
Kusini, baada ya kupatikana kwa maiti ya binadamu iliyonyofolewa myama yote.
Familia
ya Zanele Hlatshwayo, mwenye umri wa miaka 25, ambaye ametoweka tangu mwezi
Julai mwaka huu, ikiaminika kuwa ni mhasiriwa wa genge la watu wanaotuhumiwa
kula nyama ya binadamu, ambapo tayari washukiwwa watano wamekamatwa.
Mwili
wa mwanamke huyo ambo ulikuwa umeoza, ulipatikana baada ya mwanamume mmoja
kudai kuwa mganga wa kienyeji, kuamua kujisalimisha kwa polisi juma lililopita,
na kukiri kuwa amechoka kula nyama ya binadamu.
Polisi
nchini Afrika kusiri awali walipuuza taarifa hiyo.
Waliamua
kukubali taarifa hiyo baada ya mtu huyo kutoa mkono na mguu wa binadamu uliojaa
damu kama ushahidi, hapo ndipo alipokamatwa mara moja na maafisa wa polisi.
Aliwaongoza
hadi katika nyumba ya kukodishwa, ambapo polisi walipata masikio 8 ya binadamu,
ndani ya chungu cha kupikia.
Inaaminika
kuwa zingetumika kuwalisha wateja wakeambao wanaaambiwa yana nguvu za miujiza
ya kumpa mtu pesa, nguvu na ulinzi wa kutosha.
Viungo
vingine kadhaa vya mwili wa binadamu vilipatikana ndani ya mkoba
Maiti ya Bi Hlatshwayo uliojaa damu na mavazi yaliyokuwa
yameraruka, ulipatikana miongoni mwa viungo vingine vya binadamu nyumbani mwa
mganga huyo wa kienyeji.
Mavazi
ya mwanadada huyo yalitambuliwa mara moja na jamaa zake.
Hata
hivyo, polisi wangali wakisubiri matokeo ya uchunguzi wa DNA, ili kuthibitisha
ikiwa mabaki ya maiti ni ya mwanamke huyo wa mvulana wa miaka miwili.
Familia
ya Bi Hlatshwayo, bado haijamzika.
Mara
nilipoingia kwwenye maskani ya Hlatshwayo, nilisalikumbana na nyimbo za huzuni
na vilio kutoka kwa jamaa zake waliokuwa wakiomboleza
"Tunajaribu
kuwaza tu namna alivyokuwa akiomba kutoumizwa au kuuwawa muda mfupi kabla ya
kifo chake, alikufa kifo kibaya," alisema dadake mkubwa Nozipho Ntelele,
huku akifuta machozi.
"Mavazi yake yalikuwa yamefunikwa kwa nyasi na
vumbi, ambayo ni ishara tosha kuwa alipambana na wauwaji wake katika harakati
za kunusuru maisha yake," aliongeza Bi Ntelele.
Mganga huyo wa kienyeji anaishi katika nyumba moja ya
kukodisha huko Rensburgdrift karibu na mji wa Estcourt.
Jina
lake la utani ni "Mkhonyovu" inayomaanisha "Mtu mfisadi au tu
mfisadi" katika lugha ya Ki-Zulu.
Amekodisha
nyumba hiyo kutoka kwa Philani Magubane, ambaye kakake pia amekamatwa na
maafisa wa polisi, kwa kuwa mshirika wa karibu wa mganga huyo wa kienyeji.
0 comments:
Post a Comment