Wanamazingira
kutoka miji midogo ya pwani nchini Gambia wameipeleka kampuni moja ya China
mahakamani kwa madai ya kutupa takataka za sumu kwenye bahari.
Hatua
hiyo inakuja baada ya serikali kukubaliana nje ya mahakama na kampuni hiyo ya
Golden Lead kumaliza tatizo hilo.
Wakazi
wa eneo la Gunjur takribani kilimita arobaini kusini mwa mji Mkuu wa Banjul
wamesema mamia ya samaki wamekuwa wakifa katika eneo hilo la bahari tangu
kampuni hiyo ya Golden Lead ilipojenga kiwanda cha kusindika samaki katika mji
huo mwaka 2016.
Wanasema
watu ambao wamekuwa wakiogelea katika eneo hilo wamekuwa wakidhurika na kupata
matatizo ya kiafya.
Kampuni
ya Golden Lead imepinga tuhuma hizo.
Kampuni
hiyo ilikubaliana kumaliza suala hilo nje ya mahakama na Mamlaka ya taifa ya
Mazingira nchini Gambia mwezi uliopita.
0 comments:
Post a Comment