Mji
wa Lagos nchini Nigeria umeorodhwa wa pili mbaya zaidi kuishi duniani na jarida
la The Economist.
Jarida
hilo katika ripoti yake ya Global Liveability Report ya mwaka 2017,
imeorodhesha mji mkuu wa Syria, Damascus ambao umeathiriwa sana na mapigano kuwa
pekee ulio mbaya kuushinda mji huo mkuu wa kibiashara wa Nigeria.
Mji
bora zaidi kuishi duniani ni Melbourne nchini Australia.
Lagos
ni miongoni mwa miji mitano kutoka bara la Afrika ambayo imo miongoni mwa miji
10 hatari zaidi kuishi duniani.
Miji
hiyo mingine ni mji mkuu wa Libya, Tripoli, mji mkuu wa Algeria, Algiers, mji
mkuu wa Zimbabwe, Harare na mji mkubwa zaidi nchini Cameroon, Douala.
Orodha
hiyo huangazia mambo matano: uthabiti, huduma ya afya, utamaduni na mazingira,
elimu na miundo mbinu.
Kuna
mji mmoja Afrika hata hivyo ambao umeimarika pakubwa.
Abidjan,
mji mkubwa zaidi nchini Ivory Coast, uliorodheshwa kuwa miongoni mwa miji
mitano iliyoimarika pakubwa tangu kuandaliwa kwa ripoti kama hiyo miaka mitano
iliyopita.
0 comments:
Post a Comment