Mtu mmoja amefariki na wawili wamejeruhiwa baada ya gari ya
abiria kugonga treni eneo la Tanesco Morogoro.
Akidhibitisha tukio hilo Mganga Mkuu wa hospitali Frank
Jacob amesema kwamba, ajali hiyo imetokea leo asubuhi Gari hilo lilikuwa
limebeba wanafunzi lilipata ajali eneo la masika baada ya kugonga treni na
kuburuzwa umbali wa takriban mita 50 toka yalipo makutano ya reli na barabara.
Kwa upande wake Kamanda wa polisi mkoni humo Ulrich Matei,akithibitisha
kutokea kwa ajali hiyo amesema
ajali hiyo imetokea leo asubuhi na imehusisha gari aina ya daladala yenye amba
za usajili T 438 iliyokuwa inakwenda Mvumi kwenye njia panda inayoingilia
treni.
Kamanda Matei amesema chanzo cha ajali hiyo ni daladala
kuingia kwenye njia ya treni bila kusimama ili kuangalia kama kuna treni
inakuja, ndipo treni hiyo ikaburuza gari hiyo kwa umbali mrefu na kusababisha
maafa hayo.
Msikilize hapa chini kamanda wa polisi mkoani humo Ulrich Matei akielezea tukio hilo.
Msikilize hapa chini kamanda wa polisi mkoani humo Ulrich Matei akielezea tukio hilo.
0 comments:
Post a Comment