Mzungu mtetea ubabe wa wazungu ambaye akliwaua watu kwa sababu ya asili
yao miaka 30 iliyopita ameuawa kwa kudungwa sindano yenye sumu.
Mark Asay ndiye mzungu
wa kwanza katika historia ya jimbo la Florida kuuawa kwa sababu ya kumuua mtu
mweusi, kwa mujibu wa shirika linalofuatilia utekelezaji wa hukumu ya kifo.
Asay, 53, alipatikana
na hatia ya mauaji ya watu wawili mwaka 1987 katika eneo la Jacksonville.
Aliuawa saa 22:22 GMT
(saa saba na dakika 22 Afrika Mashariki).
Ilikuwa mara ya kwanza
kwa sindano yenye sumu mpya kutumiwa kumuua mfungwa.
Jopo la mahakama
liliamua Asay aliwaua waathiriwa wake - Robert Lee Booker, mtu mweusi, na
Robert McDowell, 26, mzungu wa asili ya Kilatino - kwa kuwapiga risasi usiku
ambao alikuwa ametoa matamshi ya ubaguzi wa rangi.
Waendesha mashtaka
walisema Asay alikuwa amemchukua McDowell, aliyekuwa amevalia kama mwanamke,
akashiriki naye ngono, lakini akampiga risasi baada ya kugundua jinsia yake
halisi.
Tangu kurejeshwa kwa
hukumu ya kifo mwaka 1976, watu weusi 20 wameuawa kwa makosa ya kuwaua wazungu.
Asay aliuawa kwa
kudungwa sindano yenye sumu aina ya etomidate ambayo haijawahi kutumiwa awali
Marekani.
Sumu hiyo sasa itaanza
kutumiwa badala ya sumu aina ya midazolam ambayo imeacha kutumiwa kwa sababu ya
kuwasababishia dhiki watu waliohukumiwa kuuawa wakati wanapouawa.
Etomidate
ilichanganywa na sumu nyingine mbili - rocuronium bromide na potassium acetate
- kabla ya Asay kudungwa.
Katika mahojiano na
kituo kimohc acha habari, Asay alikuwa amesema kwamba hataki kuishi jela maisha
yake yote.
Mfungwa huyo alikuwa na
chale zenye kuonyesha ubabe wa wazungu. Alikiri kumuua McDowell,lakini
akakanusha kutekeleza mauaji hayo mengine.
Alikuwa mungwa wa
kwanza kuuawa Florida katika kipindi cha miaka 18.
0 comments:
Post a Comment