Serikali ya Mkoa wa Kaskazini Unguja,
inakabiliwa na kasi ya vitendo vya udhalilishaji wa kijinsi, ikiwemo matukio ya
ubakaji na mimba kwa wanafunzi.
Hayo yalisemwa
na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Vuai Mwinyi, wakati akisoma taarifa ya
maendeleo ya Mkoa wa Kaskazini mbele ya Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein
katika ziara ya kuangalia maendeleo ya mkoa huo.
Hata hivyo Mwinyi
amesema kuwa, wameanza kudhibiti vitendo hivyo kwa kutoa elimu pamoja na kesi
hizo kusikilizwa haraka haraka katika mahakama zilizopo katika mkoa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba,
Sheria na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman alisema tayari vyombo vya sheria
ikiwemo mahakama na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka na jeshi la Polisi wamenza
kuzipatia ufumbuzi wa haraka kesi za udhalilishaji wa kijinsia.
0 comments:
Post a Comment