Utafiti
uliofanywa unaonesha kuwa watoto wa kwanza kuzaliwa katika familia huwa na
akili sana ukilinganisha na watoto wanaofuatia kuzaliwa.
Wataalamu wa Uchumi kutoka
University of Edinburgh baada ya kuwa katika mjadala kwa miaka mingi
wamehitimisha kuwa watoto wa kwanza kuzaliwa wanakuwa na kiwango cha juu cha IQ
ukilinganisha na watoto wanaowafuata.
Watafiti wanasema majibu ya
utafiti wao unaweza kuelezewa kwamba watoto wa kwanza kuzaliwa hupata mapenzi
makubwa na support kubwa katika kuendeleza akili kutoka kwa wazazi wao katika
kipindi cha miaka ya mwanzo.
Matokeo ya utafiti huo
yaliyochapishwa kwenye Journal of Human Resources, unaweza pia kuelezea
kinachoitwa athari za kuzaliwa pale ambapo ndugu wakubwa katika familia
hufurahia mshahara mzuri na elimu bora katika maisha yao ya baadaye, kwa mujibu
wa Watafiti.
Pia wameeleza kuwa wazazi wengi
hubadilika tabia pindi wanapopata watoto wengine ikiwa ni pamoja na kuwa na
muda mchache kwa ajili yao hususani kwenye kucheza nao au kuwafundisha vitu
mbalimbali.
0 comments:
Post a Comment