Mara nyingi
kumekuwa na ripoti za kuugua kwa marais, hasa rais wa Nigeria Muhammadu Buhari.
Bwana Buhari amekuwa akipokea matibabu ya ugonjwa ambao
haujulikani mjini London tangu mwezi Mei, ambayo ni ziara ya pili anafanya
kupata matibabu nchini Uingereza mwaka huu.
Lakini sasa rais wa miaka mingi wa Uganda Yoweri Museveni,
amenukuliwa akisema kuwa hajawai kuwa mgonjwa kwa miaka 31.
"Mshasikia kuwa Museveni amekuwa mgonjwa au amelazwa
hospitalini kwa miaka 31 iliyipota?" aliuliza Museveni.
"Hii ni kwa sababu ninafuata taratibu za kiafya ambazo
zimenisaidia kuizuia baaadhi ya magonjwa kama haya, mengi ya magonjwa hata
yanazuiwa."
Baadhi ya
marais ambao pia wamesafiri ng'ambo kupata matibabu tangu mwaka uliopita ni
pamoja na marais wa Angola, Zimbabwe, Benin na Algeria.
Rais wa Zimbabwe ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1980
amekosolewa na wapinzani kwa kuiongoza nchi "kutoka hospitalini"
baada ya kufanya ziara ya tatu nchini humo kupata matibabu mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment